Orodha ya ramani za nyumba zinazofaa kujengea nyumba ndogo Tanzania

Nini uhalisia wa nyumba ndogo?

Tunapokuja katika swala la ujenzi wa makazi ya kuishi familia, basi kuna mambo amabyo yamekuwa kama sheria ambayo yanaamua aina ya nyumba ambazo tunajenga. Baadhi ya mambo ni kama bajeti, tamaduni, majirani, hali ya hewa, staili… Kiujumla ktk jamii yetu tunapozungumzia nyumba ndogo tunamaanisha ni zile nyumba ambazo zinatumia nafasi ndogo ya kiwanja, zinazotumia bajeti ndogo, zilizo na urahisi kujenga n.k. Nyumba ndogo mara nyingi ni zile nyumba ambazo ukubwa wa sakafu wake upo chini ya mita za mraba 100 (sqm) na mara nyingi ni nyumba za vyumba 3 au viwili za kawaida (siyo ghorofa).

Hivyo kitaalamu nyumba ndogo ni zile nyumba ambazo zipo chini ya mita za mraba ~100 na zenye unafuu na urahisi kujenga. Maana hii inaweza badilika kutokana na mtu binafsi ambavyo anaweza kuamua. Maana hii pia inaangalizia zaidi jamii ya Kitanzania na Afrika Mashariki, hivyo kwa mtu ambaye yupo Ulaya anaweza kuta maana hii haikidhi sana.

Gharama za kujenga nyumba ndogo

Je, gharama za ujenzi za nyumba ndogo ni kiasi gani? Hili ni swali ambalo umekuwa ukihitaji kujibiwa. Kikawaida nyumba ya vyumba vitatu ya kawaida yenye ukubwa wa sakafu wa 120sqm kujenga Tanzania mpaka kuikamilisha finishing vyema ktk ubora mzuri itagharimu Tshs. ~50 – 65 Milioni, sasa tunapokuja nyumba ndogo inaweza gharimu kuanzia Tshs. 25 – 45 Milioni. Gharama hizi zinategemea sana na ukubwa haswa wa nyumba husika, staili na mtindo wa nyumba, idadi ya vyumba ktk jengo. Kujenga boma (msingi, kuta na paa) kwa nyumba hizi zinaweza kukugharimu kiasi cha Tshs. ~10 – 25 Mil kutegemeana na nyumba. Kwa Yule anayehitaji kujua gharama halisi kila nyumba ktk ramani zetu basi jiunge uanachama hapa ili uweze ona gharama kwa kila hatua ujenzi (msingi, kuta, paa, sakafu, dari, umeme…).

Sababu za watu kujenga nyumba ndogo

Zipo sababu nyingi ambazo zinaamua watu kujenga nyumba hizi ndogo na sasa tutaziangalia ili nawe uweze jihakiki kama kweli unahitaji kujenga nyumba hizi au huhitaji. Tutaangalizia pia na faida na hasara za kujenga nyumba ndogo.

  • Kuwa na bajeti ndogo kujenga

Watu wengi siku hizi wamekuwa wanataka kujenga nyumba ambazo zimejitoshereza kiuzuri lkn pia wataweza mudu gharama za ujenzi. Kutokana na kuwa na kiasi kidogo cha bajeti basi watu wengi wamekuwa wakiamua kujenga nyumba ambazo watamudu gharama lkn pia watazikamilisha vyema. Je, una Tshs. 15M na unataka kufanya ujenzi mzuri uliokamilika? Ndio inawezekana kwa kuanzia pesa hiyo kukamilisha boma la nyumba yako na ukahamia. Ijapokuwa pia ukijikita tuu kwenye gharama ndogo unaweza jikuta unaibana nyumba ikawa ndogo na ukapunguza uzuri, hivyo ni muhimu kubalance vyema bajeti na mahitaji yako. Fahamu zaidi gharama za ujenzi wa nyumba na namna ya kuokoa gharama ujenzi.

  • Eneo dogo la kiwanja

Viwanja ni gharama kununua haswa vile ambavyo vipo ktk maeneo muhimu na mazuri. Hivyo kama kiwanja chako ni kidogo na unapenda ujenge hapo basi unaweza jenga nyumba hizi ndogo vyema kabisa. Ni muhimu pia kuwa na uhalisia kama kiasi cha kiwanja hicho kitaweza kukutoshereza kwa shughuli zako zote unazotarajia ili uweze furahia nafasi yako. Fahamu zaidi aina ya kiwanja kinachofaa kununua.

  • Familia ya watu wachache

Zipo baadhi ya familia ambazo idadi ya watumiaji wa nyumba ni 3 tuu. Kuna wazee ambao wamestaafu, pia wale ambao wameamua kuishi bila kuoa aua kuolewa na labda wageni ambao unakuta wanataka nyumba ya kutosha watu wachache ambapo wanajikuta nyumba ambazo zinawafaa ni hizi za ramani ndogo. Hapa pia ni muhimu kuangalia kama idadi inaweza ongezeka au laa siku za mbeleni na kama nyumba itatosha.

  • Nyumba za kupangisha

Nyumba za kupangisha ni biashara nzuri na endelevu maana inakuletea kipato endelevu mara kwa mara kwa muda mrefu. Nyumba ya kupangisha ni uwekezaji hivyo inabidi ilete faida kwa muda wa haraka iwezekanavyo; Hivyo ni muhimu kujenga nyumba ya kupangisha ya vyumba 3 au 2 ndogo iliyojitoshereza na kutumia gharama ndogo kiujenzi ili kodi ambayo wateja watakuwa wanakulipa iweze rudisha haraka gharama yako ya ujenzi. Mtu aliyejenga nyumba kwa 30M atarudisha haraka gharama yake kuliko yule aliyetumia 50M na unaweza kuta kiasi cha pango kipo sawa. Ijapokuwa pia ni vizuri kuangalia ni aina ipi ya wateja wako unataka kuwapangisha ktk nyumba yako; je, ni wanaopenda nyumba kubwa au wanatosheka hata kwa nyumba ndogo?

  • Gharama ndogo za uendeshaji

Gharama za nyumba hazipo tuu ktk ujenzi, zipo pia ktk uendeshaji. Tunapozungumzia uendeshaji tunamaanisha kulipia gharama za usafi, matengenezo, kodi za serikali, umeme, maji, taka n.k. Hivyo kuna mwingine anataka gharama zake za kuendesha nyumba ziwe ndogo zaidi kwa kuchagua kujenga nyumba ndogo.

ID-28989
3
103 sqm
42 Pcs
17 m
2,472 Pcs
9 m
917 Pcs
ID-28880
3
100 sqm
41 Pcs
11 m
2,400 Pcs
10 m
890 Pcs
ID-28694
2
84 sqm
34 Pcs
11 m
2,009 Pcs
8 m
745 Pcs
ID-28439
2
64 sqm
59 Pcs
12 m
1,150 Pcs
5 m
572 Pcs
ID-28222
2
107 sqm
44 Pcs
12 m
2,568 Pcs
12 m
952 Pcs
ID-28041
2
96 sqm
40 Pcs
11 m
2,300 Pcs
9 m
850 Pcs
ID-27943
2
90 sqm
61 Pcs
11 m
1,600 Pcs
10 m
800 Pcs
ID-27256
3
91 sqm
39 Pcs
12 m
2,299 Pcs
9 m
853 Pcs
ID-26509
3
70 sqm
51 Pcs
11 m
1,246 Pcs
8 m
619 Pcs
ID-26508
1
35 sqm
26 Pcs
7 m
700 Pcs
6 m
315 Pcs
ID-26305
2
88 sqm
55 Pcs
11 m
1,405 Pcs
11 m
685 Pcs
ID-26278
2
77 sqm
32 Pcs
10 m
1,848 Pcs
9 m
685 Pcs
ID-22351
2
51 sqm
46 Pcs
8 m
785 Pcs
8 m
420 Pcs
ID-19705
2
61 sqm
56 Pcs
12 m
1,092 Pcs
6 m
543 Pcs
ID-19472
1
103 sqm
42 Pcs
12 m
2,472 Pcs
12 m
917 Pcs
ID-19237
0
60 sqm
25 Pcs
11 m
1,444 Pcs
6 m
536 Pcs
ID-18128
2
105 sqm
43 Pcs
11 m
2,520 Pcs
11 m
935 Pcs
ID-17760
2
68 sqm
47 Pcs
9 m
1,217 Pcs
8 m
605 Pcs
ID-17746
2
85 sqm
58 Pcs
11 m
1,522 Pcs
9 m
757 Pcs
ID-17614
2
77 sqm
53 Pcs
9 m
1,369 Pcs
9 m
681 Pcs
ID-17004
3
95 sqm
65 Pcs
12 m
1,705 Pcs
9 m
846 Pcs
ID-17013
2
89 sqm
61 Pcs
12 m
1,593 Pcs
11 m
792 Pcs
ID-17198
2
105 sqm
72 Pcs
12 m
1,880 Pcs
12 m
935 Pcs
ID-15831
1
52 sqm
27 Pcs
8 m
931 Pcs
8 m
463 Pcs

Orodha ya ramani za nyumba ndogo

Sasa hapa chini tumekupa ramani za nyumba ndogo ambazo zinafaa kujenga kwa anayehitaji kujenga nyumba ndogo na akafurahia. Ni nyumba ambazo zimeandaliwa kuangalia mazingira yetu kiuhalisia na kufuata viwango vitakavyokupa ladha nzuri ya kuzitumia.

Ramani ID-11210, vyumba 3, tofali 1096+418 na bati 50

  • vyumba 3 (1 kina bafu ndani), sebure dining jiko stoo, choo public, veranda 2
  • gharama ya kujenga boma (msingi, kuta na bati)  = Tshs~13 Mil
  • kiwanja kisipungue = 14x15m
  • ukubwa = 67sqm

Ramani ID-7780, vyumba 3, tofali 1146+860 na bati 60

Nyumba hii imeandaliwa ili iwe simple lkn pia itumie nafasi kidogo ya kiwanja chako. Staili yake ya bati haitumii bati nyingi hivyo utaweza okoa gharama ktk vifaa pia. Nyumba hii inaweza faa zaidi maeneo ya joto sababu jiko na dining vipo ktk baeaza lililo wazi. HAitumii nguzo za zege sana hivyo utaokoa gharama za zege.

  • vyumba 3 (1 kina bafu ndani), sebure dining jiko stoo, choo public, veranda 2
  • gharama ya kujenga boma (msingi, kuta na bati)  = Tshs~18 Mil
  • kiwanja kisipungue = 13x16m
  • ukubwa = 77sqm

Ramani ID-7823, vyumba 3, tofali 1200+645 na bati 65

Nyumba hii ipo zaidi kwa ukatikati kwa maana unaweza iona kama ipo kawaida lkn ina unafuu. Nyumba hii ina vyumba 3 vya kulala na sebure jiko dining na choo ndani; veranda zake zimetengenezwa kwa tofali ili usitumie zege sana na pia nyumba yote imepigwa bati hivyo utaokoa gharama sana.

  • vyumba 3 (1 kina bafu ndani), sebure dining jiko stoo, choo public, veranda 2
  • gharama ya kujenga boma (msingi, kuta na bati)  = Tshs~23 Mil
  • kiwanja kisipungue = 14x17m
  • ukubwa = 99sqm

 Ramani ID-7786, vyumba 3, tofali 830+553 na bati 62

Kijumba hiki kina ladha ya kipekee na watu wengi wamekichukua kwajili ya kujenga. Rangi na staili yake ya paa, kuta na madirisha zinawavuta wengi kujenga. Okey, ukubwa wa madirisha unaongeza gharama ujenzi lkn tumeweka hivyo ili kuleta mvuto wa nyumba. Nyumba hii inafaa kwa yule ambaye usafi kwake sio shida. Kumbuka kutumia fundi mzuri ktk kujenga nyumba hii ili uweze ifurahia mwonekano wake

  • vyumba 3 (1 kina bafu ndani), sebure dining jiko stoo, choo public, veranda 2
  • gharama ya kujenga boma (msingi, kuta na bati)  = Tshs~26 Mil
  • kiwanja kisipungue = 14x17m
  • ukubwa = 99sqm

 Ramani ID-7790, vyumba 3, tofali 1480+798 na bati 65

Jenga nyumba hii kama unahitaji ukawaida lkn ulio na unafuu ki gharama; hapa namaanisha mpangilio wa vyumba kidogo upo kikawaida lkn umebana kiasi fulani. Nyumba hii inakupa nafasi tofauti ya choo na bafu bvya public hivyo ukaweza nufaika na muingiliano wa vyumba hivyo kishughuli.

  • vyumba 3 (1 kina bafu ndani), sebure dining jiko stoo, choo public, veranda 2
  • gharama ya kujenga boma (msingi, kuta na bati)  = Tshs~22 Mil
  • kiwanja kisipungue = 14x17m
  • ukubwa = 90sqm

Ramani ID-7851, vyumba 3, tofali 1936+1088 na bati 80

Nyumba hii ina ukubwa kiasi fulani lkn bado inaangukia ktk kundi la nyumba ndogo. Ni vyumba 3 ambayo unaweza ijenga na ukaokoa gharama na nafasi ya kiwanja chako vyema. Staili la paa lake ni la kipekee na utahitaji fundi mzuri kuijenge.

  • vyumba 3 (1 kina bafu ndani), sebure, dining jiko stoo, choo public, veranda 2
  • gharama ya kujenga boma (msingi, kuta na bati)  = Tshs~24 Mil
  • kiwanja kisipungue = 17x17m
  • ukubwa = 103sqm

Ramani ID-17013, vyumba 2, tofali 1593+792 na bati 61

Hiki kijumba cha vyumba 2 ni kizuri sana na kinavuta sana kimuonekano. Ni nyumba ambayo inavyumba 2 vya kulala ambapo kimoja ni master na kingine cha kawaida. Ijenge na uweze furahia mwonekano na ladha nzuri.

  • vyumba 2 (1 kina bafu ndani), sebure dining, jiko stoo, choo public, veranda 2
  • gharama ya kujenga boma (msingi, kuta na bati)  = Tshs~21 Mil
  • kiwanja kisipungue = 15x16m
  • ukubwa = 89sqm

Ramani ID-11264, chumba 1, tofali 698+313 na bati 32

Kijumba hiki cha chumba kimoja kinafaa sana kwa yule anayependa staili simple. Unapata chumba kimoja kilicho na ukubwa wa kawaida ambapo choo utatumia cha public ambacho nacho kimekaa jirani na chumba.

  • vyumba 1, sebure dining jiko stoo, choo public, veranda 1
  • gharama ya kujenga boma (msingi, kuta na bati)  = Tshs~6 Mil
  • kiwanja kisipungue = 11x12m
  • ukubwa = 32sqm

Ramani ID-13471, vyumba 2, tofali 1389+514 na bati 61

Nyumba hii ya vyumba 2 ni special kwa yule ambaye anapenda kubarizi nje; jiko na dining vipo nje ktk veranda hivyo utakuwa unapata upepo mwanana. Ni nzuri kwa yule ambaye anajenga nyumba ktk maeneo ya joto.

  • vyumba 2 (1 kina bafu ndani), sebure, dining jiko stoo, choo public, veranda 1
  • gharama ya kujenga boma (msingi, kuta na bati)  = Tshs~17 Mil
  • kiwanja kisipungue = 13x15m
  • ukubwa = 72sqm

Ramani ID-17760, vyumba 2, tofali 1217+605 na bati 47

Nyumba ya vyumba viwili ya staili na rangi ya namna fulani. Ina sebure ambayo hapohapo unaweza tumia kwajili ya shughuli nyingine kama kupikia dining na kuhifadhi vitu. Waweza tumia kijinafasi ktk korido kuhifadhia vitu au kutumia kwa shughuli nyingine ambayo haita maliza nafasi yako.

  • vyumba 2 (1 kina bafu ndani), sebure dining jiko stoo, choo public, veranda 1
  • gharama ya kujenga boma (msingi, kuta na bati)  = Tshs~16 Mil
  • kiwanja kisipungue = 13x14m
  • ukubwa = 68sqm

Ramani ID-17004, vyumba 3, tofali 1705+846 na bati 65

Nyumba nzuri ya kipekee ya vyumba 3 ambapo chumba kimoja kina choo ndani. Ina sebure na dining vilivyo ktk sehemu moja, pia zina jiko na stoo vilivyo ktk eneo moja ila kwa kujitoshereza. Jenga nyumba hii na ufurahie rangi nzuri na mwonekano wa nyumba yako.

  • vyumba 3 (1 kina bafu ndani), sebure dining, jiko stoo, choo public, veranda 2
  • gharama ya kujenga boma (msingi, kuta na bati)  = Tshs~22 Mil
  • kiwanja kisipungue = 13x16m
  • ukubwa = 95sqm

Ramani ID-10129, vyumba 3, tofali 2024+890 na bati 33

Staili hii ya nyumba ambayo bati halionekani inaitwa contemporarty style; Nyumba hii ni ya vyumba 3 ambapo kimoja kina choo ndani. Ni nyumba kali na yenye hisia za kitofaiti ambapo utaweza ifurahia ktk kuitumia na watu wataipenda kuiona. Tumia fundi ambaye byupo vizuri sana ili uweze iona ktk uhalisia wake.

  • vyumba 3 (1 kina bafu ndani), sebure dining jiko stoo, choo public, veranda 2
  • gharama ya kujenga boma (msingi, kuta na bati)  = Tshs~30 Mil
  • kiwanja kisipungue = 15x17m
  • ukubwa =100sqm

Ramani ID-17614, vyumba 2, tofali 1369+681 na bati 53

Nyumba hii ni ya kinamna nzuri ambapo mpangilio wa vyumba vyake ndani umepangiliwa vyema na utaweza ufurahia. Ina vyumba viwili na chumba kimoja kina choo ndani. Tumia fundi mzuri kuijenga ili fundi aweze itendea haki ktk staili na mwonekano.

  • vyumba 3 (1 kina bafu ndani), sebure dining jiko stoo, choo public, veranda 2
  • gharama ya kujenga boma (msingi, kuta na bati)  = Tshs~18 Mil
  • kiwanja kisipungue = 13x14m
  • ukubwa =76.5sqm

Ramani ID-11258, vyumba 2, tofali 780+414 na bati 45

Nyumba safi ya vyumba 2 ambapo kila chumba ni cha kawaida. Ina sebure dining jiko stoo na veranda ya mbele pamoja na choo kimoja cha pamoja. Ipo simple kama ilivyo na pia ipo na gharama simple sana kuliko nyumba nyingi.

  • vyumba 2, sebure dining jiko stoo, choo public, veranda 1
  • gharama ya kujenga boma (msingi, kuta na bati)  = Tshs~9 Mil
  • kiwanja kisipungue = 12x14m
  • ukubwa =50sqm

Ramani ID-22351, vyumba 2, tofali 780+414 na bati 45

Nyumba safi ya vyumba 2 ambapo kila chumba ni cha kawaida. Ina sebure dining jiko stoo na veranda ya mbele pamoja na choo kimoja cha pamoja. Imeongezewa mwonekano fulani wa kiurembo ili kuvutia zaidi bila kubadili unafuu wake sana.

  • vyumba 2, sebure dining jiko stoo, choo public, veranda 1
  • gharama ya kujenga boma (msingi, kuta na bati)  = Tshs~11 Mil
  • kiwanja kisipungue = 12x14m
  • ukubwa =48sqm

Ramani ID-17746, vyumba 2, tofali 1522+757 na bati 58

Nyumba safi na kipekee ya vyumba 2 ambapo chumba kimoja kina choo ndani na kimoja cha kawaida. Inajengwa kwa kutumia tofali za kuchoma (waweza pia tumia tofali za cement-block au interlocking blocks). Furahia maisha mazuri na familia yako huku ukipata raha ya uhalisia wa maisha.

  • vyumba 2, sebure dining, jiko stoo, choo public, veranda 2
  • gharama ya kujenga boma (msingi, kuta na bati)  = Tshs~20 Mil
  • kiwanja kisipungue = 13x15m
  • ukubwa =85sqm

Ramani ID-15831, vyumba 1, tofali 931+463 na bati 27

Staili ya kipekee ya nyumba ambapo hapo unapata nyumba ya chumba kimoja chenye jiko na sebure. Ni nyumba ambayo imeangalia zaidi mwonekano na staili ili kukupa ladha inayofaa. Ijengee kwa kutumia fundi mzuri ili uweze ifurahia kimwonekano na staili yake original.

  • chumba 1, sebure dining, jiko stoo, choo public, veranda 1
  • gharama ya kujenga boma (msingi, kuta na bati)  = Tshs~15 Mil
  • kiwanja kisipungue = 13x13m
  • ukubwa =52sqm

Mambo ya muhimu unapotaka kujenga nyumba ndogo

Unapotaka kujenga nyumba ndogo ni muhimu kwanza ujijengee msimamo wa kuwa utaijenga nyumba hiyo katika ubora na taratibu zinazofaa bila kuchakachua kiwango cha ubora na uzuri. Ni muhimu kujenga nyumba ile ambayo unaona utaweza imudu kwa kiasi cha muda ambao umepanga kuijenga. Kumbuka kutumia wataalamu husika ikiwamo kutumia ramani kamili zenye ubora kama hizi za nyumba gharama ndogo tulizo zionesha hapa pamoja na mafundi walio na kiwango kizuri. Kumbuka kuwa nyumba ndogo haimaanishi ubora mbaya wa nyumba; unaweza jenga nyumba nzuri na ikawa nzuri na ya kuvutia sana kuliko yule aliyejenga ghorofa kwa kuchakachua.

Je, katika nyumba hizo tulizo ziorodhesha hapo juu, ni ipi ambayo inakufaa na umeipenda zaidi?

4 Responses

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

mangula
Eng. Makazi Team
Makazi.ne.tz ni mtandao mahususi Afrika Mashariki wenye lengo ...
ID-8010
4
138 sqm
108 Pcs
15 m
2,160 Pcs
13 m
1,164 Pcs
ID-18256
4
273 sqm
0 Pcs
16 m
7,956 Pcs
14 m
2,990 Pcs
ID-17704
4
287 sqm
60 Pcs
12 m
7,605 Pcs
12 m
2,383 Pcs
ID-26357
4
284 sqm
146 Pcs
18 m
5,068 Pcs
14 m
2,837 Pcs
ID-16782
4
225 sqm
155 Pcs
17 m
4,028 Pcs
15 m
2,003 Pcs
ID-15090
3
191 sqm
151 Pcs
18 m
3,419 Pcs
16 m
1,700 Pcs
ID-16993
4
169 sqm
116 Pcs
15 m
3,025 Pcs
12 m
1,504 Pcs
ID-17121
3
177 sqm
122 Pcs
15 m
3,168 Pcs
14 m
1,575 Pcs
ID-20942
5
278 sqm
115 Pcs
17 m
4,958 Pcs
13 m
2,215 Pcs
ID-17622
3
404 sqm
175 Pcs
22 m
10,725 Pcs
13 m
3,095 Pcs
ID-27394
3
169 sqm
116 Pcs
15 m
3,025 Pcs
13 m
1,504 Pcs
ID-27934
3
144 sqm
99 Pcs
14 m
2,550 Pcs
12 m
1,250 Pcs
Makazi Icon Blue

Join Membership

Join Membership to See Clear Floor Plans Before You Buy the Full Plan; See How Much MONEY is Needed to INVEST in Your Business In order to Get the Profit to Finance Construction of This House. What MORTGAGE to Borrow and Return Monthly to Your Bank. Also, See How Much it COSTS to Build the Foundation, Walling, Roofing, Ceiling, Painting, Doors, Windows… in All of Our Houses on This Platform so That You Can CHOOSE, COMPARE, PLAN & STRATEGIES on How to Approach Your Construction Rightly!