Kazi ya msingi katika nyumba

TZ
From TZS 100,000/day
Kinondoni
10 years
Mtaalamu wa mambo ya ujenzi wa makazi aliyesomea na mwenye uzoefu wa muda mrefu, kutoka kwenye kusanifu ramani za nyumba, usanifu wa nadharia ya nje ya nyumba na bustani, pamoja na mambo ya makisio na mahesabu ya gharama za ujenzi. Lengo letu ni kukuwezesha kutimiza nyumba ya ndoto yako sasa, bila kujalisha kama ni ya gharama nafuu au mjengo wa heshima.
3D Rendering Building Designing Cost Estimation Landscape Designing Project Management Project Planning Technical Drafting

Msingi ni sehemu muhimu ya jengo ambayo huunganisha jengo na ardhi husika pamoja na kupeleka mzigo wa jengo kwa usalama kabisa katika ardhi. Pasipo msingi, jengo linakuwa halijakamilika na halipo salama. Kikawaida msingi hutumia gharama kubwa katika kujenga ukilinganisha na baadhi ya maeneo katika jengo, gharama hii kubwa inaashiria umuhimu na ulazima wa sehemu hii ya jengo.

Siku zote katika tathimini ya jengo, pale inapoonekana kuwa msingi ni mbovu, basi hatua za umakini zaidi huchukuliwa maana ipo hatari inayoweza kutokea na ikaleta hasara kubwa mpaka katika maisha ya watu; ni muhimu kuwa makini katika ujenzi wa msingi wa nyumba zetu ili kuweza kupunguza hatari ambazo zinaweza kutokea na pia kuongeza thamani na afya ya jengo lako.

Ufuatao ni mchanganuo unaoonesha faida na kazi ya msingi katika nyumba ili kuweza kukuongezea ufahamu zaidi katika ujenzi wako unaofanya.

Kupunguza ukubwa wa kanieneo wa jengo

Msingi huchukua uzito wa jengo zima na kuupeleka moja kwa moja katika ardhi kwa kuugawanya uzito huo katika eneo kubwa la ardhi ili kuweza kupunguza kiasi cha kanieneo (pressure) ambacho ardhi hubeba. Hii ni sawa na kuruhusu uzito mkubwa katika eneo moja kuweza kugawanywa katika eneo kubwa zaidi ili mwisho wa siku ardhi iweze kuhimili uzito wa jengo. Hii husaidia ardhi iweze kubeba kanieneo ambayo inaweza.

Ipo athari ambayo inaweza kutokea kama ardhi ikashindwa kubeba mzigo unaoweza; ardhi ambayo inabeba uzito kuliko uwezo wake huweza kupasuka na kaharibu jengo zima. Ni sawa na kamba ambayo imebeba uzito mkubwa kuliko uwezo wake, mwisho wa siku huishia kukatika na kuangusha mzigo wa thamani. Ni muhimu kuhakikisha kuwa mzigo ambao ardhi inabeba upo ndani ya kiwango kubalika. Kwa maeneo ambayo ardhi ni mbovu, basi utaalamu zaidi huhitajika ili kuweza kutengeneza msingi wenye uwezo wa kubeba uzito wa jengo salama. Uzito wa jengo ni jumla ya uzito wa jengo lenyewe, watumiaji na uzito wa nguvu ya upepo na nguvu nyingine zinazoweza kuliathiri jengo lako.

Jengo kukaa kwa usawa katika ardhi bila kushukia upande mmoja

Katika kipindi cha muda mrefu jengo lolote hushuka ijapo kidogo katika ardhi kutokana na hali ya ‘usponji’ ya udongo; inahitajika miaka kadhaa ili jengo lisiweze kushuka chini zaidi.  Kazi mojawapo ya msingi ni kuwezesha jengo kuweza kushuka katika ardhi kwa usawa bila kulalia upande mmoja; hii huwezekana pia kwa kuugawanya uzito wa jengo kwa usawa katika ardhi hivyo kama kushuka jengo, basi lishuke kwa pamoja pande zote.

Kama jengo likishuka upande mmoja sana na kulalia upande mmoja inaweza sababisha nyufa katika jengo zima na mwisho wa siku kulifanya liweze kuwa katika hali ya ubovu.

Ijapokuwa sababu ya jengo kushuka na kulalia upande mmoja huweza sababishwa na sababu nyingine, Lakini kama msingi wa jengo lako utaweza jengwa vyema basi utasaidia kuepusha madhara mbalimbali ikiwemo kulalia upande mmoja.

Msingi huweka sehemu iliyosawa na salama ya kujengea jengo

Msingi ni muhimu sana kwa kuweka sehemu ya kujengea iwe katika usawa mmoja ili kuweza kujenga jengo lako kwa usawa (level) kabisa. Mara nyingi ardhi ambayo tumekuwa tukiichagua kujengea inakuwa haipo katika hali ya usawa, inawezekana ipo katika mteremko au katika mawe; msingi husaidia kuweza kuliweka jengo lako katika sehemu iliyo salama bila kujalisha ardhi ipoje.

Tukifanikiwa kujenga msingi katika kingo za mito, katika bahari na katika maeneo yote ambayo ni hatarishi basi inakuwa ni hatua kubwa ya kutuwezesha kuliweka jengo letu katika eneo hilo. Msingi ndio hutengeneza sakafu iliyo sawa ya kujengea jengo lako na hivyo kuweza kuruhusu kufanya shughuli mbalimbali ndani ya jengo lako bila shida wala tabu.

Msingi hulitengemaza jengo lisiteleze, lisibinuke wala kuzungukia upande mwingine

Waweza kufikiri kuhusu habari ya jengo kuteleza, kubinuka au kuzunguka – ndiyo yawezekana ikatoke katika jengo kama halijajengwa vyema. Kama jengo likipigwa na upepo upande mmoja yawezekana likasukumwa upande mwingine; au kutokana na hali ya ardhi na mambo mingine inaweza kulifanya likatelezea upande mwingine kama halijajengwa vyema.

Msingi husaidia jengo lako likae sehemu moja iliyo salama. Msingi ni kama nanga ambayo huiifunga sehemu ya juu ya jengo iweze kuwa imetengemaa vyema. Pale upepo, tetemeko la ardhi linapoipiga nyumba yako basi bado itaendelea kuwa salama.

Msingi huilinda nyumba kutoka katika athari za kuchimbwa na kulika chini

Wapo wanyama na wadudu mbalimbali ambao huchimba ardhi na kusababisha mashimo chini ya nyumba. Wadudu kama mchwa, sisimizi; wanyama kama nyoka, panya, sungura, vicheche n.k huweza sababisha mashimo chini ya nyumba; na yanaweza leta athari kama nyumba haijajengwa vyema.

Nyumba kama imejengwa katika njia ya maji, basi maji hayo yanaweza kusababisha nyumba ilike na mwisho kuweza kuanguka na kuleta athari mbalimbali.

Msingi hujengwa kwa kuhakikisha kuwa jengo lote linakuwa salama na matukio ya kulika kwa ardhi na kuchimbwa kwa mashimo katika ardhi; hii inakwenda sambamba na kuhakikisha kuwa msingi unaendelea kulindwa na kufanyiwa matengenezo katika kipindi chote cha jengo.

Mwisho, ijapokuwa kujenga msingi ni gharama, bado ni muhimu kuhakikisha kuwa jengo lako unalijenga kwa umakini na nidhamu huku ukihakikisha msingi wako umejengwa kwa kufuata taratibu za kitaalamu. Ni muhimu kuhakikisha msingi wako hauna makosa na unafanya kazi vizuri; ni pamoja na kukumbuka kufanya matengenezo mbalimbali pale inapotokea shida fulani katika msingi wako. Linda msingi wa jengo lako ili jengo liendelee kuwa imara.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

TZ
From TZS 100,000/day
Kinondoni
10 years
Mtaalamu wa mambo ya ujenzi wa makazi aliyesomea na mwenye uzoefu wa muda mrefu, kutoka kwenye kusanifu ramani za nyumba, usanifu wa nadharia ya nje ya nyumba na bustani, pamoja na mambo ya makisio na mahesabu ya gharama za ujenzi. Lengo letu ni kukuwezesha kutimiza nyumba ya ndoto yako sasa, bila kujalisha kama ni ya gharama nafuu au mjengo wa heshima.
3D Rendering Building Designing Cost Estimation Landscape Designing Project Management Project Planning Technical Drafting
ID-15370
4
255 sqm
175 Pcs
20 m
4,565 Pcs
17 m
2,270 Pcs
ID-20671
16
356 sqm
312 Pcs
29 m
6,974 Pcs
17 m
3,169 Pcs
ID-15090
3
191 sqm
151 Pcs
18 m
3,419 Pcs
16 m
1,700 Pcs
ID-18272
4
191 sqm
131 Pcs
16 m
3,419 Pcs
15 m
1,700 Pcs
ID-26446
3
191 sqm
131 Pcs
15 m
3,600 Pcs
15 m
1,700 Pcs
ID-15178
3
162 sqm
84 Pcs
15 m
3,279 Pcs
13 m
1,442 Pcs
ID-22570
4
213 sqm
146 Pcs
21 m
3,804 Pcs
12 m
1,891 Pcs
ID-15144
4
214 sqm
131 Pcs
15 m
4,340 Pcs
14 m
1,100 Pcs
ID-17565
3
184 sqm
127 Pcs
16 m
3,294 Pcs
14 m
1,638 Pcs
ID-21735
3
229 sqm
94 Pcs
17 m
5,496 Pcs
17 m
2,038 Pcs
ID-19470
2
131 sqm
0 Pcs
13 m
3,144 Pcs
11 m
1,166 Pcs
ID-21918
5
555 sqm
0 Pcs
19 m
18,101 Pcs
14 m
2,823 Pcs

Join Membership

Join our membership to become a part of our expansive platform dedicated to residential development in Africa. Gain access to house plans, informative articles, vetted builders, plot listings and construction materials!

Eng. Lwifunyo Mangula
Payment Challenges? WhatsApp Admin